1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanasheria wagoma nchini Uganda

26 Juni 2026

Wanasheria nchini Uganda wamefanya mgomo wa kususia shughuli za kisheria kama njia moja ya kupinga jinsi mwenzao Erias Lukwago alivyonyanyaswa.

Uganda Kampala 2026 | Erias Lukwago
Kiongozi wa kundi la mawakili wa kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besiegya, Erias Lukwago akizungumza na waandishi wa habari mnamo Januari 22, 2026Picha: Lubega Emmanuel/DW

Wamelezea kuwa walitaka mgomo huo wa siku moja usadifiane  na siku ya kimataifa ya kuonyesha mshikamano na wahanga wa mateso na ikiwa utawala hautatimiza matakwa yao, watatangaza hatua zingine watakazochukua wakiungwa mkono na wenzao kutoka Afrika Mashariki na bara zima la Afrika

Athari za mgomo huo wa siku moja zimehisika katika mahakama mbalimbali za nchi ambapo shughuli zimekwama kwa kuwa mawakili hawakufika mahakamani.

Kulingana na jumuiya ya wanasheria ya Uganda visa vya hivi karibuni vya kukamatwa kwa wakili mashuhuri Erias Lukwago na mahakama kukataa kumwachia kwa dhamana kutokana na hali yake ya afya baada ya kufunguliwa mashtaka sawa na mteja wake  Dkt Kizza Besigye ni kielelezo kuwa utawala haujali kukiuka sheria zinazolinda tasnia yao wala zile za haki za binadamu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW