1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanawake waandamana kudai maji Goma

6 Septemba 2019

Mamia ya wanawake wameandamana mjini Goma nchini Congo wakiitaka serikali kuongeza kiwango cha maji safi katika mji huo ili kuwawezesha kupambana na homa ya Ebola, ambayo imedumu kwa miezi 13. 

Kongo Goma Ebola Screening an der Grenze zu Ruanda
Picha: Getty Images/AFP/J. Wessels

Wanawake hao waliokuwa wamebeba ndoo za maji waliandamana katika mji huo ulioko katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo unaokaliwa na zaidi ya wakaazi milioni moja. Wakaazi wachache sana ndio wanaopata maji masafi hali ambayo imepelekea raia wengi kushindwa kupambana na janga la Ebola.

Uhabuhaa wa maji safi katika baadhi ya mitaa mjini Goma umekuwa ukisababisha mara kwa mara visa vya kipindupindu na hata wanawake wengine wakidhuliumiwa kingono wakitembea vilometa kadhaa kwakutafuta maji zoezi ambalo hadi sasasa serikali ya nchi hiyo imeshindwa kugawa maji safi na salama kwa raia wake.

Maandamano haya yamejiri siku chache tu baada ya ziara yake waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Heiko Maas mjini Goma kwa lengo la kuunga mkono juhudi za kupambana na janga la Ebola ambalo imesababisha vifo vya watu 2,000.

Chanzo: Reuters
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW