1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaItaly

Italia yakataa mageuzi ya Meloni katika kura ya maoni

24 Machi 2026

Wataliano wamesababisha pigo kubwa la kwanza dhidi ya Waziri Mkuu Giorgia Meloni kwa kukataa mageuzi yake ya mfumo wa sheria katika kura ya maoni. Meloni hata hivyo amesisitiza kuwa haendi kokote.

Waziri Mkuu wa Italia Giorgia Meloni akiwa kwenye kampeni ya kura ya maoni
Wataliano wamekataa mageuzi ya Waziri Mkuu Giorgio Meloni ya mfumo wa sheria katika kura ya maoni.Picha: Stefano Rellandini/AFP

Huku karibu kura zote zikiwa zimehesabiwa, matokeo ya kura ya maoni ya kikatiba iliyopigwa Jumapili yanaonesha upande wa "Hapana" unaopinga mageuzi hayo una asilimia 53.5, na wa "Ndiyo" ukiwa na asilimia 46.5. Karibu asilimia 59 ya wapiga kura walijitokeza ikiwa ni idadi kubwa zaidi kuliko ilivyotarajiwa. Waziri Mkuu Meloni hata hivyo amesisitiza kuwa haendi kokote. Amesema Wataliano wamezungumza na kwamba uamuzi wao utaheshimiwa, akiongeza kuwa hilo halitabadilisha dhamira yao ya kuendelea kufanya kazi kwa bidii kwa manufaa ya taifa na kuheshimu jukumu walilopewa na umma.

Wakati wa kampeni za kura ya maoni, alisema mara kwa mara kwamba kura hiyo -- ambayo ilihusu jukumu na usimamizi wa majaji na waendesha mashtaka -- haikuhusu uongozi wake mwenyewe. Lakini alifanya kampeni kali ya kuyapigia debe mapendekezo hayo, pamoja na washirika wake wa muungano katika serikali ya mrengo wa kulia, huku vyama vya upinzani vikipigania kura ya "Hapana".

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW