WASHINGTON : Mswada wa azimio la Iran waungwa mkono na Marekani
12 Desemba 2006Matangazo
Marekani imetia saini mswada wa azimio uliopendekezwa na nchi za Ulaya kuiwekea Iran vikwazo kuhusika na mradi wake wa nyuklia.Waziri wa mambo ya nje wa Marekani,Condoleezza Rice amesema,ni matumaini yake kuwa mswada huo utapitishwa kwa haraka katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.Azma ya vikwazo hivyo vinavyoweza kuanza kufanya kazi kabla ya mwisho wa mwaka huu,ni kuishinikiza Iran kuachilia mbali mradi wake wa nyuklia.