1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Washington: Waziri mkuu wa India analihutubia bunge la Marekani

19 Julai 2005

Waziri mkuu Manmohan Singh wa India amelihutubia baraza la wawakilishi na Senate ya Marekani hii leo, ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya siku tatu huko Washington. Jana alifanya mazungumzo katika Ikulu na rais George Bush. Viongozi hao wawili walizungumzia masuala ya kupanuliwa biashara kati ya nchi zao mbili na kuupiga vita ugaidi. Rais Bush alisema mkutano huo uliashiria kile alichokiita mafungamano yanayozidi ya ushirikiano baina ya Marekani na India.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW