Washington:
15 Machi 2005Matangazo
Marekani inapanga kuipatia madagascar msaada wa Dala milioni 110,kwa kipindi cha miaka minne.Kwa upande wake serikali ya Bukini imeahidi kutia njiani mageuzi ya kisiasa na kiuchumi kama inavyotakiwa na serikali ya Washington.Nchi hizi mbili zimekubaliana jinsi fedha hizo zitakavyotumika.Msaada huo utaanza kutolewa mwezi ujao,mara tuu mkataba utakapotiwa saini.Madagascar ni nchi ya kwanza kupatiwa msaada kama huo wa maendeleo ,ulioanzishwa na utawala wa rais George W. Bush.
