Washukiwa wawili wa ugaidi wakamatwa
18 Januari 2008Matangazo
Polisi nchini Kenya wamewakamata raia wawili wa kigeni, mjerumani na mholanzi kwa tuhuma za kuhusika na vitendo vya ugaidi. Raia hao wawili wanadai ni waandishi wa habari.
Polisi wamewatia mbaroni Andrej Hermlin Leder, mwenye pasi ya kusafiria ya Ujerumani, na Gerduwe Sleur van Dissel, aliyekuwa na pasi ya kusafiria ya Uholanzi, katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi wakati walipokuwa wakijaribu kuondoka nchini humo jana usiku.