1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wataalamu wa UN wasema kundi la IS lazidi kujiimarisha Mali

26 Agosti 2023

Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wamesema katika ripoti yao mpya kwamba, kundi la dola la kiislamu limeongeza mara mbili idadi ya maeneo inayoyadhibiti nchini Mali ikiwa ni chini ya mwaka mmoja.

Symbolbild islamischer Staat Fahne
Picha: CPA Media/picture alliance

Wapinzani wa kundi hilo wanaofungamanishwa na kundi la kigaidi la Al Qaida wametumia nafasi iliyoachwa wazi kujiimarisha, kufuatia kile kinachoonekana kuwa udhaifu wa makundi yaliyojihami yaliyotia saini mkataba wa amani wa mwaka 2015. 

Wataalamu hao wamesema mkwamo wa utekelezwaji wa makubaliano ya amani hasa katika masuala ya upokonywaji wa silaha, uhamasishaji na ujumuishwaji wa watu hao katika jamii, umelipa nguvu kundi hilo la Jama'a Nusrat ul-Islam wa al-Muslimin linalojulikana kama JNIM kupigania uwongozi Kaskazini mwa Mali.  

Wataalamu hao wamesema, mashambulizi na vurugu hasa zinazosababishwa na wapiganaji wa IS katika eneo la sahara pia zimefanya mkataba huo wa amani kuwa dhaifu na usioaminika na maafisa wa usalama waliotarajiwa kulinda jamii zinazoshambuliwa. 
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW