1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAsia

Watu 126 wafa kwenye mafuriko na maporomoko Nepal

Hawa Bihoga
29 Septemba 2024

Maafisa nchini Nepal wamesema watu wasiopungua 126 wamekufa na wengine 64 hawajulikani walipo, kufuatia mafuriko yaliosababishwa na mvua za msimu na maporomoko ya udongo nchini humo.

Nepal | Watu wakivuka kwa kamba.
Watu wakiokolewa kwa kamba kufuatia mafuriko NepalPicha: Subaas Shrestha/IMAGO/NurPhoto

Mvua hizo zilizoanza Alhamisi jioni, zimesababisha uharibifu mkubwa nchini humo, hasa katika mikoa ya mashariki na kati.

Kulingana na msemaji wa polisi wa Nepal, Dan Bahadur Karki, watu 73 wamejeruhiwa vibaya katika mikoa mbalimbali tangu Ijumaa.

Soma pia:Zaidi ya watu 59 wafariki nchini Nepal kufuatia mafuriko

Zaidi ya nusu ya vifo vilitokea katika mji mkuu wa Kathmandu na wilaya zinazouzunguka mji huo, zilizoathirika pakubwa na mafuriko na maporoko ya udongo.

Vyombo vya habari nchini humo vimezielezea mvua mjini Kathmandu kuwa ndiyo mbaya zaidi katika kipindi cha miongo kadhaa.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW