1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 16 wauawa katika shambulizi la Israel, Gaza City

17 Septemba 2025

Mashambulizi ya usiku kucha ya Israel katika ukanda wa Gaza, yamewaua takriban watu 16. Kwa mujibu wa maafisa wa hospitali ya Shifa katika ukanda huo, wanawake na watoto ni miongoni mwa watu hao waliouawa.

Wapalestina wa Gaza wakimbia Gaza City kwa kutimia magari na kwa miguu huku wakibeba mali zao mnamo Septemba 17, 2025
Wapalestina wa Gaza wakimbia Gaza CityPicha: Abdel Kareem Hana/AP Photo/picture alliance

Maafisa hao pia wamesema zaidi ya nusu ya waathiriwa, waliuawa katika mashambulizi dhidi ya Gaza City, akiwemo mtoto na mama yake waliokuwa nyumbani mwao katika kambi ya wakimbizi ya Shati.

Katikati mwa Gaza, hospitali ya Al-Awda imesema kuwa shambulizi la Israel lililenga nyumba moja katika kambi ya wakimbizi ya Nuseirat na kuwauwa watu watatu ikiwa ni pamoja na mwanamke mjamzito.

Hata hivyo jeshi la Israel halikujibu mara moja ombi la tamko kuhusu mashambulizi hayo.

Wakati huo, muungano wa mashirika makubwa ya misaada, leo umeihimiza jumuiya ya kimataifa

kuchukua hatua kali kukomesha mashambulizi ya Israel Gaza City, baada ya  tume ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa kugundua kuwa Israel inafanya mauaji ya kimbari Ukanda wa Gaza.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW