1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan Kusini

Watu 18 wauawa Sudan Kusini kufuatia mzozo wa ardhi

7 Februari 2024

Majambazi wenye silaha wamewaua watu 18 wakiwemo wanajeshi wanane magharibi mwa jimbo la Bahr el Gazal nchini Sudan Kusini.

Sudan Kusini | Mwanamke akiwa katika mji ulio karibu na Juba
Mwanamke akiwa katika kambi ya wakimbizi karibu na mji mkuu wa Sudan Kusini wa Juba: 08.06.2022Picha: Ryoji Fukasawa/Yomiuri Shimbun/picture alliance

Hayo ni kulingana na Gavana wa muda wa jimbo hilo Arkenjelo Anyar ambaye amesema kuwa baadhi ya watu waliuliwa kwa kuchomwa moto.

Majambazi hao kutoka jimbo jirani la Warrap waliteketeza kwa moto eneo la soko, makazi ya raia pamoja na kituo cha polisi huko Tharkueng Payam kufuatia mzozo wa ardhi. Wanawake, watoto na wazee ni miongoni mwa waliouawa huku watu wengine zaidi ya 2,000 wakilazimika kuyahama makazi yao.

Jumatano iliyopita, watu 39 waliuawa na makumi ya wengine walijeruhiwa kufuatia ghasia zilizozuka kati ya makundi hasimu ya wafugaji katika majimbo ya Warrap na yale yaliopo katikati mwa nchi hiyo.  Sudan Kusini  ni moja ya nchi masikini zaidi duniani licha ya kuwa na rasilimali ya mafuta.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW