1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Moto wauwa watu 30 kwenye kituo cha mafuta Urusi

15 Agosti 2023

Watu wasiopungua 30 wamekufa baada ya kituo cha mafuta kushika moto na kusababisha mlipuko mkubwa katika jimbo la kusini mwa Urusi la Dagestan

Russland Dagestan | Explosion einer Tankstelle
Picha: Russian Emergencies Ministry in the Republic of Dagestan/REUTERS

Mbali ya idadi hiyo ya vifo, mkasa huo kwenye mji mkuu wa jimbo hilo la kusini mwa Urusi wa Makhachkala umewajeruhi wengine 105 ikiwemo watoto 15.

Wizara ya Huduma za Dharura nchini Urusi imesema moto huo ulizuka majira ya usiku kwenye kituo kimoja cha kutengeneza magari na kisha kusambaa hadi kwenye kituo cha mafuta kilicho jirani na kusababisha mlipuko wa kutisha.

Picha na mikanda ya video vilionesha moto mkubwa ukiwaka na jengo moja la ghorofa likitetekea wakati vikosi vya zima moto vikijaribu kupambana kuuzima.

Kufuatia mkasa huo, rais Vladimir Putin ametuma salamu za rambirambi kwa familia za wahanga na amewatakia afua ya haraka wote wanapatiwa matibabu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW