1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 33 wauawa kwenye shambulizi la wanamgambo Nigeria

20 Februari 2026

Takriban watu 33 wameuawa baada ya wanamgambo wa itikadi kali kufanya mashambulizi kwenye wilaya moja kaskazini magharibi mwa Nigeria. Haya ni kulingana na msemaji wa polisi, Bashir Usman.

Waasi washambulia shule moja ya upili nchini Nigeria na kuwateka nyara wanafunzi
Maafisa wa jeshi nchini Nigeria washika doria katika eneo la Kankara mnamo Desemba 16, 2020Picha: Sunday Alamba/AP Photo/picture alliance

Katika taarifa aliyoitoa jana jioni, Usman amesema shambulizi hilo lilifanyika katika jamii ya Biu jimboni Kebbi.

Usman ameongeza kuwa washambuliaji hao walivuka kutoka jimbo la Sokoto, ambalo sehemu zake zinakaliwa na kundi la waasi la Lakurawa na kwamba uchunguzi wa awali unathibitisha kuwa waasi hao wenye silaha waliingia eneo hilo kuiba ng'ombe.

Hata hivyo ameongeza kuwa maafisa wa usalama wametumwa ili kurejesha na kudumisha utulivu.

Kundi la Lakurawa linafanya shughuli zake kaskazini magharibi mwa Nigeria, hasa karibu na jamii katika jimbo la Sokoto. Kundi hilo lenye silaha linajulikana kwa wizi wa mifugo, uvamizi wa vijiji na utekaji nyara ili kupata kikomboleo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW