Watu 70 wauawa katika machafuko Syria:
14 Machi 2004Matangazo
DAMASKUS/GÖTTINGEN: Watu wapatao 70 wameuawa yalipotokea machafuko kati ya Wakurdi na maafisa wa usalama huko Syria ya Kaskazini. Shirika la Kupigania Haki za Umma Zinazokandamizwa liliarifu mjini Göttingen, Ujerumani kuwa wanajeshi wa Syria walizingira eneo zima kati ya nchi tatu Syria, Iraq na Uturuki. Inasemekana katika mji wa Kamishli vifaru vya Kisyria vilishambulia raiya wa Kikurdi. Katika miji ya Alleppo na Damaskus wanafunzi wa Kikurdi walifanya maandamano ya kupinda hatua hizo za wanajehi wa Syria.
