Janga
Mafuriko yawauwa watu 8 Kenya, safari za ndege zavurugika
7 Machi 2026
Matangazo
Licha ya juhudi hizo, Mkuu wa Polisi jijini Nairobi George Seda ametahadharisha kwamba idadi ya vifo huenda ikaongezeka. Mvua kubwa zilianza kunyesha Ijumaa na kuendelea usiku kucha hali iliyosababisha magari kufunikwa na maji. Kiwango hicho kikubwa cha maji ya mvua pia kimeripotiwa kusababisha uharibifu kwa zaidi ya magari 100.
Safari za ndege zaathiriwa
Kutokana na mafuriko hayo, Safari za Shirika la Ndege la Kenya Airways zimevurugika na huenda hali hiyo ikaendelea kwa muda mrefu zaidi. Jeshi nchini humo limepelekwa kusaidia shughuli ua uokoaji ili kuwafikia wakaazi waliokwama katika maeneo mbalimbali.