Watu 81 wapoteza maisha kufuatia mafuriko Kenya
23 Machi 2026
Mamlaka nchini Kenya jana zimefahamisha kwamba mvua kubwa ambayo imekuwa ikiendelea kunyesha nchini humo na kuleta mafuriko imesababisha vifo vya takriban watu 81 ndani ya mwezi huu.
Mamlaka ya Kenya pia imesema mvua hizo zinaendelea kunyesha katika maeneo mengi ya nchi hiyo huku kanda ya Magharibi ikiathirika vibaya zaidi ambako baadhi ya vijiji vimezamishwa kabisa katika kaunti ya Kisumu na eneo la mashamba la hekari 1,200 likiharibiwa na mimeo kusombwa.
Watu 66 wapoteza maisha kutokana na mafuriko Kenya
Zaidi ya familia 3,000 zimelazimika kuyahama makaazi yao katika eneo la Nyakach,baadhi wakipata hifadhi kwenye vituo vinane vilivyowekwa kusadia waathika, wakati maji yanayomwagika kutoka mto Mirui yakiendelea kusababisha kitisho kwa jamii ya maeneo hayo.
Mamlaka pia zimesema mji mkuu Nairobi ndio ulioshuhudia vifo vingi vya watu 37 kufuatia mafuriko.