1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu bilioni moja kupewa chanjo ya homa ya manjano Afrika

12 Aprili 2018

Umoja wa Mataifa utaendesha kampeni ya kutoa chanjo dhidi ya homa ya manjano barani Afrika. Kampeni hiyo inalenga watu bilioni moja ifikapo 2026

Afrika Kongo Gelbfieber Impfung
Picha: Reuters/K. Katombe

Takriban watu bilioni moja barani Afrika watapewa chanjo dhidi ya homa ya manjano ifikapo mwaka 2026 katika kampeni inayoendeshwa na Umoja wa Mataifa yenye lengo la kutokomeza homa hiyo barani Afrika.

Virusi vinavyosababisha homa ya manjano vinavyosambazwa na mbu huuawa watu wengi barani humo na husambaa haraka katika maeneo yanayokaliwa na watu wengi.

Akizindua kampeni hiyo ya chanjo nchini Nigeria, Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema sindano moja tu ya chanjo hiyo ya kinga dhidi ya homa ya manjano itamlinda mtu dhidi ya ugonjwa huo kabisa.

Nigeria hivi sasa inakabiliwa na mripuko wa homa ya manjano huku mamia ya watu wakiripotiwa kuathirika tangu mwezi Agosti. Nusu ya idadi ya waathiriwa ni watoto.Miongoni mwa nchi zinazotajwa na WHO kuwa katika hatari kubwa ya kuwa na mripuko wa homa ya manjano ni Sudan, Sudan Kusini, Uganda na Jmahuri ya kidemokrasia ya Congo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW