1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiMarekani

Dunia yaomboleza kifo cha gwiji wa muziki, Tina Turner

Daniel Gakuba
25 Mei 2023

Mwanamuziki maarufu na mtumbuizaji wa mtindo wa Rock & Roll Tina Turner aliyeshirikiana na mume wake Ike Turner miaka ya 1960 na 1970 kutoa nyimbo zilizoenziwa kote duniani, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 83.

USA Anaheim | Tina Turner
Picha: Rose Prouser/REUTERS

Kulingana na meneja wake, Turner aliyekuwa na uraia wa Uswisi tangu mwongo mmoja uliopita, amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu katika makaazi yake ya Küsnacht karibu na mji wa Zurich. Wimbo wake maarufu zaidi ulikuwa "What's Love Got to Do." Mbali na kuwa malkia wa muziki, Turner alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza maarufu duniani kuzungumzia udhalilishaji wanaopitia wanawake majumbani.

Salamu za rambirambi zinaendelea kutumwa kutoka kote ulimwenguni kutoka kwa wasanii, mashabiki na hata viongozi wa nchi akiwemo Rais wa Marekani Joe Biden aliyesema kuwa Turner alikuwa na kipaji kilichobadilisha milele muziki wa Marekani.

''Juu ya kuwa na kipaji adimu kilicholeta mabadiliko ya kudumu katika muziki wa Marekani, Tina alikuwa ni mtu imara, aliyeshinda vikwazo chungu nzima, na manyanyaso, na kujenga fani itakayodumu kwa vizazi vingi na kuacha urithi ambao ni wake binafsi,'' limesema tangazo la Rais Biden kuhusiana na kifo cha Tina Turner.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW