Watu saba wauawa katika machafuko Uganda
16 Januari 2026
Matangazo
Ghasia zimeripotiwa katika maeneo ya Butambala, ambako polisi na mbunge wa eneo hilo walitoa maelezo yanayokinzana kuhusu chanzo cha vifo hivyo.
Polisi walisema kundi la wafuasi wa upinzani lilishambulia kituo cha polisi, huku mbunge Muwanga Kivumbi akidai kuwa watu waliuawa ndani ya nyumba yake walipokuwa wakisubiri matokeo ya uchaguzi wake.
Matokeo ya awali yanaonyesha Museveni anaongoza kwa zaidi ya asilimia 75, huku mpinzani wake Bobi Wine akidai udanganyifu mkubwa na kutangaza kuwa vikosi vya usalama vilikuwa vimezingira nyumba yake.