1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiAfghanistan

Watu 17 wafariki Afghanistan kufuatia mafuriko

Saleh Mwanamilongo
29 Machi 2026

Mvua kubwa, mafuriko na maporomoko ya ardhi nchini Afghanistan yamesababisha vifo vya watu 17. Watu wengine 26 wamejeruhiwa kwenye maafa hayo yaliyotokea saa 24 zilizopita.

Afghanistan, Ghor 2024 | Nyumba zilizoharibiwa baada ya mafuriko makubwa katika jimbo la magharibi la Afghanistan
Mvua kubwa, mafuriko na maporomoko ya ardhi nchini Afghanistan yamesababisha vifo vya watu 17Picha: Omid Haqjoo/AP Photo/picture alliance

Kwa mujibu wa mamlaka, majimbo 13 miongoni mwa 34 ya nchi hiyo yameathirika, hasa maeneo ya magharibi, kati na kaskazini-magharibi mwa Afghanistan.

Zaidi ya nyumba 140 zimeharibiwa, kilomita zipatazo 80 za barabara zimesombwa na maji, huku mashamba na mifumo ya umwagiliaji pia vikiharibiwa.

Zaidi ya kaya 500 zimeathirika. Mamlaka zimesema, idadi ya vifo inaweza kuongezeka huku tathmini ikiendelea, na mvua zaidi inatarajiwa katika siku zijazo.

Raia wametakiwa kuondoka kutoka kwenye maeneo ya mito yaliyo hatarini kukumbwa na mafuriko. Afghanistan inaendelea kukabiliwa na majanga ya hali mbaya ya hewa yanayochangiwa na mabadiliko ya tabianchi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW