1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Watu wasiopungua 24 wameuwawa kwa shambulio la droni Sudan

8 Februari 2026

Watu wasiopungua 24 wameuawa baada ya shambulio la droni lililotokea karibu na mji wa Rahad, Kordofan Kaskazini nchini Sudan siku ya Jumamosi. Watoto 8 ni miongoni mwa watu waliouwawa.

Khartoum, Sudan 27.08.2023
Moshi ukifuka kutokana na mapigano nchini SudanPicha: Wang Hao/XinHua/picture alliance

Kulingana na Shirika la Mtandao wa madaktari wa Sudan, shambulio hilo lilililenga gari lililokuwa limezibeba familia za watu waliolazimika kuyakimbia makazi yao, kutokana na machafuko. Watu wengine kadhaa ambao idadi yao haijatajwa wamejeruhiwa na walipelekwa hospitali mjini Rahad.

RSF washutumiwa kuhusika na shambulio

Kundi la wanamgambo wa Rapid Support Forces (RSF) linadaiwa kuhusika na shambulizi hilo, siku moja baada ya jingine lililoulenga msafara wa wahisani kutoka Shirika la Mpango wa Chakula Duniani WFP. Wanamgambo hao wanaopambana na jeshi rasmi la Sudan, hawajatoa kauli yoyote kuhusiana na tukio hilo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW