MigogoroUkraine
Watu watano wauawa Ukraine kufuatia mashambulizi ya Urusi
5 Oktoba 2025
Matangazo
Wanne kati ya hao wameuawa katika jimbo la Lviv linalopakana na Poland ambayo ni mwanachama wa NATO. Serikali ya Poland imesema imetuma ndege za kivita mapema leo katika eneo hilo la mpakani ili kuhakikisha usalama wa anga lake.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema Urusi imefanya mashambulizi makubwa ya makombora zaidi ya 50 na droni karibu 500. Maelfu ya watu wamesalia bila umeme katika jimbo la kusini mashariki la Zaporizhzhia ambako kumeripotiwa pia kifo cha mtu mmoja.
Urusi haijazungumzia chochote kuhusu shambulio hilo lakini katika siku za hivi karibuni, imezidisha mashambulizi yake na kuilenga miundombinu ya nishati ya Ukraine hasa wakati huu msimu wa baridi ukikaribia.