1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Zaidi ya watu 300 watekwa nyara Nigeria

7 Machi 2026

Kundi la wanamgambo wenye itikadi kali limewakamata na kuwateka nyara zaidi ya watu 300 nchini Nigeria. Wanamgambo hao waliushambulia mji wa Ngoshe ulio kwenye jimbo la Borno la Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.

Nigeria Kuriga 2024 | Jeshi likilinda eneo la shule walikotekwa wanafunzi katika jimbo la Kaduna
Wanajeshi wakilinda doria baada ya moja ya matukio ya watu kutekwa nyara nchini NigeriaPicha: Sunday Alamba/AP Photo/picture alliance

Mamlaka zimesema huenda shambulio hilo ni la kulipiza kisasi kutokana na operesheni ya jeshi iliyowauwa makamanda watatu wa kundi la Boko Haram. Hadi sasa hakuna kundi lolote lililokiri kuhusika na tukio hilo. 

Mashambulizi mengine yazuiwa na polisi

Msemaji wa jeshi Uba Sani, amesema wanajeshi walifanikiwa kuyazuia mashambulizi mengine ya aina hiyo yaliyoshuhudiwa katika jamii za  Konduga, Marte, Jakana, na  Mainok kati ya Jumatano na Ijumaa wiki hii.

Nigeria inakabiliwa na kitisho cha usalama kutokana na makundi kadhaa ya wanamgambo wenye itikadi kali yakiwemo Boko Haram, ISWAP, Lakurawa na mengine yenye makao yake katika Ukanda wa Sahel.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW