Waumini 163 watekwa nyara kanishani Nigeria
20 Januari 2026
Taarifa zilizotolewa siku ya Jumatatu (Januari 19) zilisema kuwa washambuliaji hao waliyavamia makanisa hayo na kuwalazimisha waumini hao kuondoka nao kuelekea maporini.
Ripoti hizo zilithibitishwa na vyanzo mbalimbali, akiwemo mkuu mmoja wa kanisa, chifu wa kijiji na Umoja wa Mataifa.
Hata hivyo, polisi ya jimbo hilo ilikataa kuthibitisha matukio hayo ilipoombwa na shirika la habari la AFP.
Mashambulizi hayo ya Jumapili ni ya hivi karibuni kabisa katika wimbi la utekaji nyara unaofanywa na magenge yaitwayo majambazi katika taifa hilo la magharibi ya Afrika, ambao huwalenga Wakristo na Waislamu, kwa ajili ya kudai fedha za kikomboleo.
Mnamo mwezi Novemba, magenge hayo yaliwateka zaidi ya wanafunzi na walimu 300 kutoka skuli moja ya Kikatoliki, ambapo 50 walifanikiwa kukimbia na wengine kuachiliwa kwa mikupuo miwili wiki kadhaa baadaye.