1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Waziri Mkuu Mpya wa Ufaransa Sebastien Lecornu ajiuzulu

6 Oktoba 2025

Waziri Mkuu wa Ufaransa Sebastien Lecornu aliyeteuliwa hivi karibuni amejiuzulu Jumatatu katika hali ambayo haikutarajiwa.

Paris | Waziri Mkuu wa Ufaransa aliyejiuzulu Sebastien Lecornu
Waziri Mkuu wa Ufaransa aliyejiuzulu Sebastien Lecornu akizungumza mjini ParisPicha: Eliot Blondet-Pool/SIPA/picture alliance

Ikulu ya Elysée imesema barua ya kujiuzulu ya Lecornu imewasilishwa kwa rais Emmanuel Macron ambaye ameukubali uamuzi huo.

Hatua ya  Lecornu  kujiuzulu imejiri ikiwa ni saa chache baada ya kuteua baraza lake jipya la mawaziri, ambapo nafasi nyingi muhimu ziliendelea kushikiliwa na mawaziri waliokuwepo.  Kabla ya hatua ya Waziri mkuu huyo kujiuzulu, upinzani walitishia kuiangusha serikali yake, jambo linalodhihirisha ni jinsi gani kuna mzozo na mkwamo mkubwa wa kisiasa nchini Ufaransa.

Siasa za Ufaransa ziliingia kwenye misukosuko tangu  rais Macron alipochaguliwa tena kwa muhula wa pili mwaka 2022 na zilivurugika kabisa baada ya uchaguzi wa mapema wa Bunge wa mwaka jana ambapo hakuna chama chochote kilichofanikiwa kupata wingi unaohitajika wa wabunge.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW