BiasharaCanada
Waziri Mkuu wa Canada kuzuru India kurekebisha uhusiano
24 Februari 2026
Matangazo
India ni kituo cha kwanza cha Carney kwenye ziara yake ya Asia-Pasifiki inayojumuisha pia mataifa ya Australia na Japan, akilenga kupunguza utegemezi kwa Marekani.
Carney amesema mfumo wa ulimwengu kuongozwa na Marekani unapotea taratibu na kwa maana hiyo Canada haipaswi kutegemea kwamba huenda utarejea baada ya Rais Donald Trump kuondoka.
Waziri Mkuu huyo anaondoka Alhamisi kwenda India, kwa ziara itakayofuatiliwa kwa karibu wakati yeye na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi watakapokuwa wanajaribu kurekebisha uhusiano ambao ulivunjika mwaka 2024.