1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Fumio Kishida akumbuka ukoloni wa Japan kwa Korea Kusini

7 Mei 2023

Waziri mkuu wa Japan Fumio Kishida anayefanya ziara Korea Kusini ametoa kauli ya kuonesha huruma juu ya ukoloni wa Japan nchini Korea ya Kusini. Wakati wa ukoloni huo watu wa Korea Kusini walifanyishwa kazi za kitumwa

Südkorea Seoul | Präsident Yoon Suk Yeol (R) und Premierminister Kishida Japan
Picha: Jung Yeon-je/AFP/AP/picture alliance

Waziri mkuu Kishida na mwenyeji wake rais Yoon Suk Yeol wa Korea Kusini, wamesisitiza azma ya kusuluhisha mivutano ya miaka iliyopita na kuimarisha ushirikiano baina ya nchi zao, katika muktadha wa changamoto inayotokana na mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini.

Soma zaidi:Korea Kusini yathibitisha kurejesha mahusiano ya kijeshi na Japan

Waziri mkuu wa Japan amesema yeye  binafsi ana machungu moyoni juu ya watu waliokabiliwa na mazingira magumu wakati wa ukoloni. Hata hivyo hakuomba radhi kwa kauli ya uwazi. Waziri mkuu huyo wa Japan ameanza ziara ya siku mbili nchini Korea Kusini baada ya rais wa Korea Kusini kufanya ziara nchini Japan katikati ya mwezi wa Machi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW