1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSudan

Waziri Mkuu wa Sudan ataka UM uunge mkono mpango wa amani

23 Desemba 2025

Waziri Mkuu wa Sudan, Kamil Idris, amelitolea mwito Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuunga mkono mpango wa amani kwa taifa lake lililoharibiwa kwa vita.

Sudan Port Sudan 2025 | Waziri Mkuu wa Sudan, Kamil Idris
Waziri Mkuu wa Sudan, Kamil Idris.Picha: Ibrahim Adaroub/Xinhua/picture alliance

Akizungumza kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Idris amesema mpango wa usitishaji vita unahitajika haraka iwezekanvyo chini ya usimamizi wa Umoja huo, ule wa Afrika na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu.

Amesisitiza mpango huo ni sharti uwalazimishe wanamgambo wa RSF kuondoka kwenye maeneo wanayoyashikilia na kisha kuruhusu kuundwa serikali ya mpito itakayoandaa uchaguzi huru nchini Sudan.

Kwa zaidi ya miaka miwili sasa, Jeshi la Sudan linapambana na vikosi vya wanamgambo wa RSF katika mzozo ambao umesababisha vifo vya maelfu ya watu na kuwalazimisha mamilioni kukimbia miji yao.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW