1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Waziri mkuu wa Ufaransa akemea uhalifu wa waandamanaji

24 Machi 2023

Waziri mkuu wa Ufaransa Eisabeth Borne amesema kadhia iliyoshuhudiwa wakati wa maandamano ya nchi nzima jana Alhamisi ya kupinga mageuzi ya pensheni hayakubaliki.

Frankreich Rentenüberarbeitung | Premierministerin Elisabeth Borne
Picha: Bertrand Guay/AP Photo/picture alliance

Hali inazidi kuwa tete katika baadhi ya miji nchini humo. Borne ameandika kupitia ukurasa wa twitter akisema wana haki kuandamana na kuwasilisha madai yao lakini akaonya kwamba vurugu na uharibifu ulioshuhudiwa jana havikubaliki.

Soma pia: Maandamano yaendelea Ufaransa kupinga mpango wa mageuzi ya pensheni

Waziri wa mambo ya ndani Gerald Darmanin amesema zaidi ya askari 150 wa vikosi vya usalama wamejeruhiwa na zaidi ya watu 170 wamekamatwa. Kulingana na wizara hiyo zaidi ya watu milioni 1 waliandamana ingawa taarifa nyingine zinasema karibu watu milioni 3.5 walishiriki maandamano hayo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW