Waziri Mkuu wa Ukraine akutana na waziri wa jeshi la Marekan
20 Novemba 2025
Matangazo
Yulia ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake katika jukwaa la mtandao wa kijamii.
Amesema ziara hiyo inatoa fursa muhimu kwa maafisa wakuu wa jeshi wanaoongozana na waziri huyo kutathmini hali ilivyo Ukraine na kushuhudia moja kwa moja matokeo ya uchokozi wa Urusi.
Jana, Driscoll na ujumbe wa maafisa wakuu wa kijeshi wa Marekani, alikutana na mkuu wa jeshi la Ukraine.
Ukraine yapokea miili ya wanajeshi
Wakati huo huo, Ukraine imeipokea miili 1,000 ya kile ambacho Urusi imesema ni askari wake waliouawa.
Kituo cha kuratibu masuala ya wafungwa wa kivita cha Kiev, kimesema leo kuwa wachunguzi kutoka vyombo vya sheria, na mashirika ya kitaalamu ya Wizara ya Mambo ya Ndani, hivi karibuni watafanya uchunguzi wote muhimu na kuitambua miili hiyo iliyorejeshwa nyumbani.