Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga afariki dunia
15 Oktoba 2025
Matangazo
Hospitali ya Devamatha katika jimbo la Kerala imethibitisha taarifa za kifo chake hivi leo. Odinga ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 80, aliwahi kugombea urais wa Kenya mara tano katika kipindi cha zaidi ya miongo mitatu.
Mwezi machi, Raila Odinga alikuwa amesaini makubaliano ya kisiasa na rais wa sasa William Ruto ambayo yalikiruhusu chama chake cha upinzani cha ODM kushiriki katika mchakato muhimu wa kupitisha sera huku baadhi ya wanachama wake wakiteuliwa kuwa mawaziri.
Rais Ruto anatarajiwa kulihutubia taifa na kukitangaza rasmi kifo cha Odinga. Viongozi mbalimbali duniani wameanza kutuma salamu zao za rambirambi.