Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Nepal akamatwa na polisi
28 Machi 2026
Matangazo
Msemaji wa polisi wa Kathmandu, Om Adhikari amesema mamlaka zimechukua hatua hiyo ili kuchunguza jukumu la mawaziri hao wa zamani katika maandamano ya kupinga ufisadi yaliyofanyika mwezi Septemba mwaka jana na yaliyosababisha vifo vya zaidi ya raia 70.
Jopo la serikali lapigilia msumari kukamatwa Oli na Lekhak
Hayo yanajiri siku kadhaa baada ya jopo lililoteuliwa na serikali kupendekeza wawili hao washtakiwe kwa tuhuma za uzembe katika kuyasimamia maandamano hayo.
Oli na Lekhak wamekamatwa siku moja baada ya Waziri Mkuu mpya Balendra Shah kuapishwa. Maandamano katika taifa hilo la Kusini mwa Asia yaliyofanyika mwaka uliopita yaliyoongozwa na vijana maarufu kama Gen Z yaliuangusha utawala wa Oli na yalichochewa na hatua ya serikali kupiga marufuku mitandao ya kijamii.