1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri wa mambo ya kigeni wa Kenya kuizuru Urusi

11 Februari 2026

Waziri wa mambo ya kigeni wa Kenya Musalia Mudavadi atasafiri na kuelekea Moscow mwezi ujao, kufuatia sakata la Wakenya kulaghaiwa na kujiunga na jeshi la Urusi katika vita vya Ukraine.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Kenya, Musalia Mudavadi
Waziri wa mambo ya kigeni wa Kenya, Musalia MudavadiPicha: Sebastian Gollnow/dpa/picture alliance

Mudavadi amesema kuwa katika ziara yake hiyo, atafuatilia na kuhakikisha kuachiwa kwa Wakenya wanaoshikiliwa kama wafungwa wa kivita nchini Ukraine na kufahamu pia hali ya wale walio mahospitalini.

Waziri huyo amesema zaidi ya Wakenya 30 wamerejeshwa nyumbani kutoka Urusi katika kipindi cha siku miezi miwili iliyopita na mashirika feki ya ajira kufungwa katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.

"Ombi letu kwa serikali ya Urusi ni kuhakikisha Wakenya hawako katika orodha ya wanaotarajiwa kusajiliwa. Tunataka hilo liwe wazi kabisa," alisema Mudavadi.

Ripoti katika wiki kadhaa zilizopita zinaonesha kuwa Wakenya waliolaghaiwa kwenda Urusi kufanya kazi zenye malipo ya juu, wanafariki dunia katika uwanja wa mapambano na kupata majeraha mabaya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW