1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya wataka kuwalinda zaidi wakimbizi wa Ukraine

15 Septemba 2023

Waziri wa mambo ya ndani wa Ujerumani Nancy Faeser amesema anaunga mkono pendekezo la kuongeza muda wa hadhi ya ulinzi ndani ya Umoja wa Ulaya kwa wakimbizi kutoka Ukraine.

Maafisa wa zimamoto wakiwasaidia wakimbizi wa Ukraine walipowasilia Romania Machi 25,2022 walipokimbia uvamizi wa Urusi nchini mwao
Maafisa wa zimamoto wakiwasaidia wakimbizi wa Ukraine walipowasilia Romania Machi 25,2022 walipokimbia uvamizi wa Urusi nchini mwaoPicha: Anca Gheonea/ABACA/picture alliance

Nancy Faeser ameyasema hayo katika mahojiano yaliyochapishwa leo kwenye magazeti ya Ujerumani ya shirika la Funke Mediengruppe.

Waziri huyo wa mambo ya ndani wa Ujerumani ameeleza kuwa, hivi karibuni atajadili juu ya suala hilo na mawaziri wengine wa mambo ya ndani wa Umoja wa Ulaya.

Mnamo siku ya Jumatano, Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen alipendekeza kuongeza muda wa hadhi ya ulinzi ndani ya Umoja wa Ulaya kwa wakimbizi wa Ukraine.

Mataifa ya Umoja wa Ulaya yaliamua kuwapa hadhi maalum raia wa Ukraine wanaotafuta hifadhi ndani ya EU kufuatia uvamizi kamili wa Urusi mnamo Februari, mwaka 2022.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW