Wadephul ziarani Syria kuimarisha ushirikiano
30 Oktoba 2025
Matangazo
Ni katika ziara ya kwanza ya Wadephul nchini Syria baada ya ziara mbili za mtangulizi wake Annalena Baerbock ambaye mwezi Machi alifungua ubalozi wa Ujerumani mjini Damascus.
Ushirikiano wa kisiasa, uchumi na masuala ya kiutu kuimarishwa
Taarifa iliyotolewa na wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani imesema mazungumzo hayo yanalenga kuimarisha ushirikiano wa kisiasa, kiuchumi na masuala ya kiutu.
Itakumbukwa kuwa Ujerumani iliwapokea maelfu ya wakimbizi kutoka Syria wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa kipindi cha miaka 14. Akiwa na ujumbe wake, Wadephul anatarajiwa kuelekea Lebanon na Bahrain katika ziara yake Mashariki ya Kati.