Wenger awaomba mashabiki kuiunga mkono timu
15 Mei 2017Mojawapo ya timu zinazowania nafasi hiyo ni Arsenal na kocha Arsene Wenger amewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi kesho Jumanne katika mechi yao dhidi ya Sunderland badala ya kushiriki katika mgomo unaolenga kumshinikiza na kuharakisha kuondolewa kwake kama kocha wa miamba hao wa London.
Kocha huyo wa muda mrefu hatangaza kama atabwaga manyanga au atabaki uwanjani Emirates wakati mkataba wake wa sasa utakamilika baada ya mwisho wa msimu.
The Gunners wana mechi tatu tu zilizobaki kabla ya msimu kukamilika, mbili katrika Premier League dhidi ya Sunderland na Everton kabla ya fainali ya FA dhidi ya mabingwa wapya na mahasimu wao wa London Chelsea.
Taarifa ya mashabiki kwenye mtandao wa onlinegooner.com iliashiria kuwa kocha wa Atletico Madrid Diego Simeone au wa Juventus Maximilliano Allegri wanaweza kujaza viatu vya Wenger.
Mwandishi: Bruce Amani/AFP
Mhariri: Iddi Ssessanga