1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Usalama wa chakulaSudan

WFP kupunguza mgawo wa chakula Sudan kuanzia Januari 2026

12 Desemba 2025

Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula limesema litapunguza mgawo wa chakula kwa jamii za nchini Sudan zinazokabiliwa na njaa kutokana na upungufu wa fedha.

Sudan Tawila 2025 | Wakimbizi kutoka kambi za Zamzam katika kambi ya muda
Watu waliokimbia kambi ya Zamzam kwa ajili ya wakimbizi wa ndani baada ya kuangukia chini ya udhibiti wa RSF, wakipanga foleni kwa ajili ya mgao wa chakula magharibi mwa Sudan Aprili 13, 2025.Picha: AFP

Mkurugenzi wa masuala ya Dharura wa WFP Ross Smith amewaambia waandishi wa habari nchini Geneva leo Ijumaa kwamba kuanzia mwezi Januari watapunguza mgawo kwa asilimia 70 kwa jamii zenye njaa na asilimia 50 kwa wale wanaokabiliwa na kitisho cha njaa.

Jamii katika eneo la Darfur zimekumbwa na njaa na utapiamlo kufuatia mzingiro wa RSF kwenye eneo la Al-Fashir uliodumu kwa miezi 18.

Vita vilivyozuka mwaka 2023 kati ya jeshi la Sudan na wanamgambo wa RSF vimesababisha kile ambacho Umoja wa Mataifa umekitaja kama mgogoro mbaya zaidi wa kibinaadamu duniani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW