1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

WFP kupunguza msaada wa Chakula kwa watu 750,000 Somalia

3 Oktoba 2025

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula, WFP, limetangaza kuwa lina mpango wa kupunguza msaada wa chakula kwa maelfu ya watu nchini Somalia ifikapo mwezi Novemba mwaka huu.

WFP imetangaza kupunguza msaada wa chakula kwa watu 750,000 mwezi Novemba
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula, WFPPicha: Abukar Albadri/dpa/picture-alliance

WFP limesema idadi ya watu wanaopokea msaada wa dharura wa chakula itapunguzwa kutoka milioni 1.1 hadi watu 350,000 katika mwezi wa Novemba kutokana na ukosefu mkubwa wa fedha za ufadhili. Mamilioni ya watu wanakabiliwa na athari mbaya zinazosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi na baa la njaa nchini Somalia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW