1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WHO yaridhia chanjo mpya ya malaria kwa watoto

3 Oktoba 2023

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limeridhia chanjo ya pili ya ugonjwa wa malaria kwa watoto, ambayo inaweza kuokoa maisha ya maelfu endapo kutakuwa na uwezekano wa kuziba pengo kubwa la usambazaji na mahitaji.

Indien | Treffen der G20-Gesundheitsminister | Tedros Adhanom Ghebreyesus
Picha: Ajit Solanki/AP/dpa/picture alliance

Takriban watoto nusu milioni katika kanda ya Afrika hufa kila mwaka kutokana na ugonjwa huo unaosababishwa na vimelea vinavyoenezwa na mbu.Mkuu wa Shirika la Afya Duniani Tedros Adhanom Ghebreyesus amenukuliwa akiseama "Kama mtafiti wa malaria, nilikuwa na ndoto ya siku ambayo tutakuwa na chanjo salama na yenye ufanisi dhidi ya malaria. Sasa tuna mbili."Chanjo mpya aina ya R21/Matrix-M, iliyoendelezwa na Chuo Kikuu cha Oxford cha Uingereza na kutengenezwa na taasisi ya Serum ya India, tayari imeidhinishwa kutumika nchini Burkina Faso, Ghana na Nigeria.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW