1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WHO yaapa kubakia Gaza

11 Septemba 2025

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema wafanyakazi wake wataendelea kubakia kwenye Jiji la Gaza licha ya miito ya jeshi la israel kuwataka watu wahame kwenye kitovu hicho cha Ukanda wa Gaza.

Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus.
Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus.Picha: Christopher Black/World Health Organization/AFP

Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Tedros Adhanom Ghebreyesus, alisema siku ya Jumatano (Septemba 10) kwamba shirika lake limefadhaishwa na amri hiyo ya  kuwataka watu milioni moja  kwenda kwenye kiitwacho na jeshi la Israel "eneo salama la kibinaadamu ambalo kiuhalisia halipo."

Mkuu huyo wa WHO alisema nusu ya hospitali zinazoendelea kufanya kwenye Ukanda huo zipo ndani ya Jiji la Gaza na "Ukanda huo hauwezi tena kupoteza vituo zaidi vya afya."

Msimamo wa WHO ulitolewa wakati jeshi la Israel likiendelea kuyaporomosha majengo makubwa kwenye Jiji hilo, likidai kuharibu vituo vya mawasiliano na mashambulizi vya kundi la Hamas.

Ndani ya kipindi cha masaa 24 yaliyopita, Israel imewauwa  Wapalestina 70  kwenye mashambulizi hayo. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW