SiasaUganda
Wine akiri yuko mafichoni, akiukimbia utawala wa Museveni
23 Januari 2026
Matangazo
Wine ameiambia DW kwamba wanajeshi waliagizwa na Mkuu wao Muhoozi Kainerugaba, mtoto wa Rais Yoweri Museveni aliyepambana naye kwenye uchaguzi wa wiki iliyopita na ambaye anaamini alimshinda.
Bobi Wine amesema anahofia usalama wake huku akiishutumu familia ya rais kwa kuchukua hatua kinyume cha sheria, akiongeza kuwa wanafanya wanachokitaka na tayari amearifiwa kwamba wanataka kumdhuru.
Mwanasiasa huyo amesema, hakuna na namna nyingine zaidi ya kujificha kwa kuwa hakuna taasisi yoyote ambayo ingeweza kumlinda.