1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Witkoff kufanya mazungumzo Berlin kuhusu Ukraine

13 Desemba 2025

Mjumbe Maalum wa Marekani Steve Witkoff anatarajiwa kufanya ziara kueleka Berlin kukutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky na viongozi wengine wa Ulaya huku shikinizo la mpango wa amani kwa Ukraine likiendelea.

Saudi-Arabia Riadh 2025 | Steve Witkoff
Mjumbe Maalum wa Marekani Steve Witkoff Picha: Evelyn Hockstein/AFP

Afisa mkuu huko Washington amelithibitisha shirika la habari la dpa kwamba Witkoff atasafiri kuelekea Berlin wikendi hii kwa mkutano huo lakini hakutoa maelezo zaidi kuhusu mfumo wa mazungumzo hayo.

Wakati huohuo, kansela wa Ujerumani Friedrich Merz, anatarajiwa kukutana na Zelensky na viongozi kadhaa wa Ulaya ikiwa ni pamoja na wakuu wa Umoja wa Ulaya na jumuiya kujihami ya NATO siku ya Jumatatu.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer pia wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo utakaofanyika katika majengo ya ofisi ya Kansela huyo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW