1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Witkoff na Kushner kukutana na Putin kujadili vita vya Ukrai

2 Desemba 2025

Mjumbe maalum wa Rais wa Marekani Donald Trump, Steve Witkoff atakutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin leo kwa mazungumzo ya kusitisha vita vya Ukraine.

USA Washington D.C. 2025 | Treffen zwischen Wolodymyr Selenskyj und Donald Trump im Weißen Haus
Picha: Presidential Office of Ukraine/SvenSimon/picture alliance

Kulingana na msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov, mazungumzo hayo kati ya Putin na Witkoff yatafanyika mchana wa leo.

Afisa mmoja wa ikulu ya White House amesema mkwewe Trump Jared Kushner ataungana na Witkoff katika ziara yake hiyo nchini Urusi.

Putin amesema mara kadhaa kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo ya amani ila iwapo Ukraine itakataa makubaliano, basi vikosi vya Urusi vitasonga mbele na kuyateka maeneo zaidi.

Haya yanafanyika wakati ambapo viongozi wa Ulaya wameonyesha mshikamano na Rais Volodymyr Zelenskiy, baada ya mazungumzo ya Marekani na Ukraine ya kupitia upya pendekezo la amani ambalo awali lilikuwa linaipendelea Urusi.

Zelenskiy ambaye leo atakuwa anakutana na rais wa Ireland na kulihutubia bunge nchini humo, hapo jana alikutana na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na baada ya kikao chao wakaungana na viongozi wengine wa Ulaya ikiwemo Ujerumani, Italia na Uingereza kwa njia ya simu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW