Palestina: Israel yasababisha vifo Ukingo wa Magharibi
21 Novemba 2025
Katika taarifa yake, wizara hiyo imesema vijana waliouwawa ni Amr Khaled Ahmed Al-Marbou aliye na umri wa miaka 18, na Sami Ibrahim Sami Mashayekh aliye na umri wa miaka 16.
Jeshi la Israel pamoja na polisi wanaodhibiti eneo hilo hadi sasa hawajasema lolote kuhusu tukio hilo na wala kujibu ombi la shirika la habari la AFP, kuwataka watoe maoni yao juu ya mauaji hayo. Kulingana na shirika la hilali nyekundu lililowapeleka vijana hao hospitalini, wote wawili waliovalia vesti ya kujikinga na risasi walijeruhiwa vibaya vifuani.
Adi al-Shurfa, ambae ni rafiki ya Al Marbou aliyeshuhudia kisa hicho amesema wote wawili walikuwa nje wakati wa machafuko kati ya jeshi la Israel na raia wa Palestina, kabla ya kupigwa risasi. Amesisitiza rafiki yake hakuwa anarusha mawe wala kushiriki katika machafuko hayo.