"Ulaya haijajiandaa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi"
17 Februari 2026
Matangazo
Ulaya inapaswa kuongeza uwekezaji wake haraka ili kuwalinda watu na miundombinu kutokana na mafuriko, moto wa nyika na joto kali. Hayo yameelezwa leo na washauri wa Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) waliotahadharisha kuwa mabadiliko ya tabianchi yameifanya Ulaya kuwa bara lenye joto kali zaidi duniani.
Takwimu za Umoja wa Ulaya zinaonyesha kuwa gharama za uharibifu wa miundombinu na majengo barani Ulaya kutokana na hali mbaya ya hewa umekadiriwa kufikia dola bilioni 53.34 kwa mwaka, hii ikiwa ni mara tano zaidi kuliko miaka ya 1980.