1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Yanga yamtimua kocha licha ya kuendelea kushinda

7 Mei 2026

Yanga wamemtimua kocha Pedro Goncalves licha ya ushindi mwingine wa ligi uliowaweka kileleni bila kupoteza mchezo. Timu hiyo inaongoza kwa pointi tano dhidi ya Simba.

Tanzania | Picha ya pamoja ya timu ya Young Africans Sports Club
Kocha Pedro Goncalves ameinoa Yanga kwa miezi saba tu na haikufungwa chini ya uongozi wakePicha: Mhindi Joseph

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Young Africans S.C. maarufu kama Yanga, wamemtimua kocha wao raia wa Ureno licha ya timu hiyo kuendelea kuongoza ligi bila kupoteza mchezo hata mmoja msimu huu.

Hatua hiyo imekuja baada ya Yanga kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC Jumatano, ushindi uliowasogeza karibu zaidi kutetea ubingwa wao wa tano mfululizo.

Mashabiki ya Klabu ya YangaPicha: Mhindi Joseph

Katika taarifa fupi, klabu hiyo ilisema tu kuwa imeachana na Goncalves na kumshukuru kwa mchango wake ndani ya timu, bila kueleza sababu za kuondolewa kwake.

Kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Angola alikuwa ameinoa Yanga kwa miezi saba pekee lakini aliisaidia kuendelea kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi tano dhidi ya watani wao Simba S.C.

Mbali na mafanikio ya ndani ya nchi, Goncalves pia aliiongoza Yanga kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mara ya nne katika historia ya klabu hiyo, ingawa walishindwa kufika robo fainali.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW