1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaYemen

Zaidi ya mataifa 30 yametoa ahadi ya msaada wa kibinadamu

28 Februari 2023

Zaidi ya mataifa 30 yametoa ahadi ya msaada wa kibinadamu wa karibu Euro bilioni 1.2 katika mkutano wa UN mjini Geneva unaolenga kuwasaidia raia wa Yemen baada ya miaka minane ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.

USA UN-Sonderbeauftragter Martin Griffiths
Picha: Xie E/Xinhua News Agency/picture alliance

Mratibu wa Misaada ya Dharura wa Umoja wa Mataifa, Martin Griffiths ametoa wito wa kuendelea na muda wa kuwekwa chini silaha akionesha kuwepo kwa nafasi ya kusitishwa kabisa mapigano.

Grifitths amesema kiwango cha fedha kilichotolewa cha dola bilioni 1.2 sio kile kilichotarajiwa cha dola bilioni 4.3 lakini Umoja wa Mataifa umesema huenda dola bilioni 2 zikapatikana mwishoni mwa wiki hii katika mkutano huo wa wahisani wa kuhamasisha utoaji wa msaada kwaajili ya Yemen.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW