1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zaidi ya nusu idadi ya watu Sudan wanahitaji msaada

15 Novemba 2025

Zaidi ya nusu ya idadi ya watu wa Sudan wanahitaji msaada wa kibinadamu. Hayo yameelezwa na Mkuu wa Baraza la Wakimbizi la Denmark, huku mapigano yakiliharibu taifa hilo la kaskazini mashariki mwa Afrika.

Charlotte Slente
Katibu Mkuu wa Baraza la Wakimbizi la Denmark Charlotte SlentePicha: Danish Refugee Council

Wiki hii, Katibu Mkuu wa Baraza hilo la Wakimbizi la Denmark Charlotte Slente ameliambia shirika la habari la AFP baada ya ziara yake katika eneo la mpakani mwa Chad na Sudan kwamba alishuhudia hali ambayo zaidi ya watu milioni 30 wanahitaji msaada wa kibinadamu, hiyo ikiwa ni nusu ya idadi jumla ya watu wa Sudan na kusisitiza kuwa "mateso aliyoyashuhudia hayafikiriki."

Sudan inashuhudia ukiukwaji unaovunja sheria zote za kimataifa

Ameongeza kusema eneo hilo linashuhudia ukiukwaji unaovunja sheria zote za kimataifa za kibinadamu na kwamba shirika hilo limeona ushahidi wa mauaji ya watu wengi na unyanyasaji wa kingono nchini Sudan.

Pia amesema watu wamewekwa kizuizini, kutekwa nyara, kulazimishwa kukimbia na mateso

Slente ameishtumu jamii ya kimataifa kwa kutochukuwa hatua za kutosha kuhusu Sudan.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW