ZANZIBAR: Hotuba za wabunge kwanza zipitiwe na spika
2 Agosti 2006Matangazo
Wanachama wa chama kikuu cha upinzani kisiwani Zanzibar siku ya Jumanne walitoka nje wakati wa kikao cha bunge,baada ya mbunge wa upinzani kukatazwa kusoma hotuba ambayo hapo kabla haikuhakikiwa na spika wa bunge.Mwezi uliopita, wabunge waliarifiwa na spika Pandu Ameir Kificho kupeleka hotuba zao katika ofisi yake kuhakikiwa kabla ya kuzisoma bungeni,ili kuzuia kile alichokiita”matamshi ya uchochezi yanayoweza kusababisha mvutano.”