1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Zelenskiy akosoa matokeo ya mkutano wa Geneva

19 Februari 2026

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amekosoa matokeo ya mazungumzo ya siku mbili mjini Geneva kati ya wawakilishi wa Ukraine na Urusi, akisema hayakufikia matarajio.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskiyPicha: Valentyn Ogirenko/REUTERS

Rais huyo wa Ukraine alikuwa anataka mazungumzo hayo miongoni mwa mambo mengine yaangazie uwezekano wa kufanyika kwa mkutano kati yake na Rais Vladimir Putin.

Putin amesema mazungumzo kama hayo yanaweza kufanyika ila mjini Moscow tu, jambo ambalo Zelenskiy amelipinga.

Zaidi ya hayo Zelenskiy anasema alikuwa ameyataka mazungumzo hayo ya Geneva yajikite katika kuangazia masuala ya kiutu kama ubadilishanaji wa wafungwa na raia.

Marekani kupitia msemaji wa ikulu ya White House Karoline Leavitt kwa upande wake imesema kumekuwa na hatua muhimu zilizopigwa kwenye mazungumzo hayo, huku kukiwekwa ahadi za ushirikiano katika kupata makubaliano ya amani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW