Zelenskiy akosoa matokeo ya mkutano wa Geneva
19 Februari 2026
Matangazo
Rais huyo wa Ukraine alikuwa anataka mazungumzo hayo miongoni mwa mambo mengine yaangazie uwezekano wa kufanyika kwa mkutano kati yake na Rais Vladimir Putin.
Putin amesema mazungumzo kama hayo yanaweza kufanyika ila mjini Moscow tu, jambo ambalo Zelenskiy amelipinga.
Zaidi ya hayo Zelenskiy anasema alikuwa ameyataka mazungumzo hayo ya Geneva yajikite katika kuangazia masuala ya kiutu kama ubadilishanaji wa wafungwa na raia.
Marekani kupitia msemaji wa ikulu ya White House Karoline Leavitt kwa upande wake imesema kumekuwa na hatua muhimu zilizopigwa kwenye mazungumzo hayo, huku kukiwekwa ahadi za ushirikiano katika kupata makubaliano ya amani.